Sunday, 4 March 2018

JIFUNZE MITI YENYE UWEZO MKUBWA 01

Tags

Miti inayo tuzunguka, ina nguvu nyingi sana za kiroho. Ukiwa na ufahamu juu ya nguvu za kiroho zinazopatikana ndani ya miti mbalimbali, basi maisha yako ya hapa duniani yatakuwa rahisi sana. Leo nitaelezea miti michache pamoja na nguvu za kiroho iliyo nazo. Unga wa alovera. Huwekwa kwenye chupa maalumu na kufukiwa ama kuzikwa kaburini kwa ajili ya kuwanyamazisha watu wanao zungumza uongo na uovu kuhusu wewe. Unga wa muagrimonia : Unga huu ni moja kati ya dawa zenye nguvu kubwa sana za kiroho, kazi yake kubwa ni kurudisha laana na uchawi kwa mtu aliye utuma kwako. Unga wa mualfafa.

Huwekwa nyumbani kujilinda dhidi ya umasikini na kufilisika, pia huwekwa kwenye chombo maalumu na kisha kwenda nao benki au kwa mtu yoyote Yule kwa ajili ya kupata mkopo wa fedha. Unga wa Mvuaza : Hutumika kwa ajili ya kumpumbaza mtu au kuwapumbaza watu. Husaidia pia kujilinda dhidi ya majambazi na kushinda kesi Unga wa mfausiku : Una matumizi mengi sana si rahisi kuyataja yote hapa. Unga wa mti wa mlufakale. Hutumika kurefusha umri wa kuishi. Hutumiwa sana na wachawi na ndio sababu wachawi wengi huishi miaka mingi sana. Hutumika katika biashara, mapenzi, mahusiano, kazi, uongozi na kadhalika, kwa ajili ya kudumisha jambo lililokusudiwa, yaani kama ni ndoa basi iwe ya kudumu na kama ni mapenzi yawe yadumu na yasife na kama ni biashara iwe ya kudumu na isife. Unga wa mualikani: Kazi kubwa ya dawa hii ni kukomesha uchawi uliotumwa kwako kwa ajili ya kukutia umasikini, kukufilisi au kukusababishia matatizo ya kifedha.

Ngekewa : Ngekewa sio mti, ni manyoya ya mnyama apatikanae porini, mnyama huyu hufanana na Ndezi, au Panya Buku. Manyoya ya mnyama huyu hutumika kuvuta wateja katika biashara na kuongeza bahati katika mambo mbalimbali kama vile sanaa na kadhalika, Unga wa Viungo vya aina zote kama vile karafuu, pilipili manga n.k. matunda mbegu na matunda jamii ya karanga : Hutumika katika tambiko maalumu la kuleta mafanikio katika biashara, pamoja na kuongeza bahati katika biashara . Unga wa mualtea Hutumika kuwaita malaika wazuri katika nyumba, pamoja na kuongeza uwezo wa mtu wa kiroho ama wa kuona mambo yaliyo rohoni. Kwa mfano kama kuna siri Fulani kuhusu mtu Fulani (mathalani mke au mume wako ) unataka kuijua, unachotakiwa ni kutumia unga huu huku ukifanya manuizo maalumu, usiku wa siku hiyo utaonyeshwa siri unazo taka kuzijua kupitia ndoto.

Pia hukupa uwezo wa kun'gamua mahali vilipo vitu vilivyo potea, utakupa uwezo wa kujua mambo yanayo tokea sehemu nyingine. Kwa mfano, wewe unaishi Dar Es salaam, na familia yako inaishi Mbeya, unaweza kujua mambo yanayo endelea huko kupitia nguvu ya unga huu. . Muangelica : Unga wa mti huu husaidia kuwalinda wanawake pamoja na watoto dhidi ya uovu wowote. Wanawake wajawazito wanashauriwa kutumia unga unga huu ili kujilinda dhidi ya jicho ovu. . Muanisi : Ni unga unaotumika kumkinga mtu dhidi ya jicho ovu na uchawi.

MSHALESHALE : Ukichanganywa na unga unga wa kiberiti, unga wa mti huu una nguvu za jabu sana kwa watu wanao jihusisha na kamari pamoja na bahati nasibu. . KINYESI CHA SHETANI : Unga unga wa mti huu unatumika katika kujikinga na kujiepusha na magonjwa mbalimbali, kujikinga dhidi ya laana na ulozi, pamoja na kusaidia katika kesi. . UNGA WA MBAMUGILE : Husaidia kuwapatanisha wapenzi walio achana na kuwafanya wasiachane tena. . UNGA WA MBABELI : Hutumika kuumwaga katika njia wanazo pita adui zako na kuwafanya wasikutafute tena. Ni dawa nzuri sana ya kujikinga dhidi ya maadui. Hutumika pia kwa kuchanjia. . MNYOKA MWEUSI : Unaitwa mnyoka mweusi kwa sababu unakopatikana porini huwa na umbo kama la nyoka mweusi. Ni miongoni mwa miti yenye nguvu kubwa sana za kiroho ( spiritual powers ). Husaidia kutoa ulinzi na pia hutumika katika uponyaji. Watu wengi wanaotumia miujiza ya uponyaji hutumia mti huu hapa. Una uwezo wa kuponya magonjwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na yale ya kichawi.


EmoticonEmoticon