Sunday, 4 March 2018

JIFUNZE MITI YENYE UWEZO MKUBWA 02

Tags

MFILIMBIBARAKA :
Huchanganywa na maji na kisha kuzungushiwa kwenye nyumba kwa ajili ya kuiepusha nyumba na uchawi/wachawi na watu waouvu kama vile majambazi nakadhalika. Hutumika kuhamisha nyumba kichawi nyakati za usiku. Mara nyingi hutumiwa na watu wanao fanya kazi za ulinzi. Husaidia pia kuwapumbaza watu wanao kuja kufanya uovu nyumbani kwako. Hawataiona nyumba yako, wataipitiliza au hawatafika kabisa.

MDAMUDAMU : Husaidia kuimarisha uhusiano kati ya ndugu wa damu. Hutumika pia katika kiapo cha kuwaweka pamoja wanandoa au wapenzi wanao taka kuingia katika ndoa.

MMBULUKOSHI : Hutumika kuwalinda watu pamoja na nyumba dhidi ya uovu na watu wabaya.

MMBULUBENDERA : Hutumika kulinda mashamba dhidi ya wanyama waharibifu pamoja na wachawi.

MBODODO : Husaidia kuwarudisha mapepo wabaya kwa mtu aliye watuma, kukukinga dhidi ya mapepo wabaya na uchawi wa aina yoyote ile, pia kuwazuia watu usio wahitaji wasije kwako. Vile vile katika biashara hukusaidia kuwazuia wateja wabaya (bad customers ) wasije kwenye biashara yako. Hapa maana yake ni kwamba, utakuletea wateja w azuri tu , yaani wateja wenye uwezo wa kununua bidhaa zako ama kumudu gharama ya huduma zako. ( WATEJA WABAYA NI WATEJA WASIO WEZA KUNUNUA BIDHAA ZAKO AMA WALE WASIO WEZA KUMUDU GHARAMA ZA HUDUMA YAKO ).

MNYOKA MWEUPE : Huitwa MnyokaMweupe kutoka na kutengeneza umbo kama la nyoka, uwapo porini kabla hauja vunwa. Kazi yake kuu ni kutoa magonjwa ya kurogwa, kutoa vitu vichafu tumboni ( kama umelishwa vitu vichafu ). Pia ukichanjiwa mti huu inasaidia kukukinga dhidi ya nyoka. Vilevile kama unaishi kwenye eneo ambalo kuna majani mengi, unashauriwa kumwaga unga unga wa mti huu walau mara moja kwa wiki, hii husaidia kuwakimbiza nyoka.

MBORAGUA : Hutumika kujenga amani, upendo na ushirikiano katika familia, pia huifanya nyumba kuwa yenye amani, na kuvutia wageni wazuri. MRIJAUFAGIO : Kazi kubwa ya mti huu ni kuondoa uchawi na wachawi kwenye nyumba, kuwafukuza na kuwazuia wageni wasio hitajika nyumbani pamoja na kukulinda na uovu.

MKALAMUSI a.k.a MKATAKESI : Mti huu una uwezo na nguvu za ajabu sana katika kuwasaidia watu kushinda kesi mahakamani au kazini. MKALENDULA : Kazi ya mti huu kama ilivyo kwa MKALAMUSI ni kusaidia kushinda kesi mahakamani pamoja na kuongeza uwezo kutoa unabii na kuona mambo yaliyo fichika ukiwa ndotoni.

MKARAWEI : Hutumika katika kutoa ulinzi pamoja na kuwalinda watoto wadogo dhidi ya uovu na uchawi na kuwafanya wakue vizuri. . MKADAMONI : Hutumika kumfanya mtu asiye mpenzi wako avutiwe kimapenzi na wewe, na atamani kufanya mapenzi na wewe. . MKASKARA: Husaidia kuleta na kuongeza bahati njema na pia kukusaidia kushinda kesi mahakamani.

MKATINIPU : Hutumika kuukamata moyo na nafasi ya mpenzi wako na kumfanya kuwa mtumwa kwako. . MSIDA : Hutumika katika kuchora alama maalumu kwa ajili ya kumfanya mtu asiye hitajika aondoke kwa amani bila kukubughudhi. Mti huu hutumika katika uchawi maarufu uitwao SUKNHU ambao hutumiwa sana na wazigua huko mkoani Tanga. Katika uchawi huu kama kuna mtu ahitajiki mahali, basi litafanywa tambiko maalumu kwa ajili ya kumfanya mtu huyo aondoke mwenyewe bila kufukuzwa. . MSELENDINI : Hutumika kuimarisha nguvu na maono ya kiroho na pia kukupa uwezo wa kuota ndoto za kinabii ama kuona mambo yaliyo fichika kupitia ndoto au kuona mambo yatakayo tokea baadaye kupitia ndoto.

Kama wewe ni mtu unaye safari mara mara kwa mara unashauriwa kuwa na unga wa mti huu, kwani utakusaidia kubaini kama safari yako itakuwa salama ama si salama siku moja kabla ya safari. . MMANZANILA : Hutumika katika kamari na bahati nasibu. . MCHERIGAMBA : Husaidia katika kuimarisha upendo, mahaba, mvuto wa kimapenzi na unyumba. . Mdalasini : Husaidia kuusafisha mwili na kuongeza bahati na mvuto. . MCHIA : Husaidia kuzuia usengenyaji pamoja na kuwabaini watu wanao kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. ( wanafiki ) . MDAMIANA : Hutumika kumpata mpenzi mpya, kuimarisha mvuto wa kimapenzi pamoja na kumrudisha mpenzi aliye ondoka.

1 coment�rios so far

kama ungependa kuokoa uhusiano/ndoa yako basi nitakupendekeza kwa Dk Dawn. alinisaidia kurejesha nyumba yangu baada ya miezi 11 ya utengano mkali kati yangu na mume wangu. Nilielekezwa kwake na dada yangu mkubwa wakati ndoa imeisha, akarudisha amani na furaha katika ndoa yangu, pia amesaidia marafiki zangu wengine na wanaishi kwa furaha kwa msaada wa Dk Dawn,
Wasiliana naye ikiwa unahitaji usaidizi wa kurejesha uhusiano/ndoa yako/ ikiwa unataka kupata mimba au kuponya aina yoyote ya ugonjwa:
Dk Dawn hatawahi kukukatisha tamaa:
Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com
WhatsApp: +2349046229159


EmoticonEmoticon