MKUNAZI – MTI KIBOKO YA MAJINI NA MASHWETANI
Unaweza ukajiuliza Mkunazi ni nini? Je, ni sababu zipi zikaufanya mti huu kuwa wa kipekee tofauti na mingine? Unapoongelea Mkunazi ni ule mti ambapo Allah ameuita Sidrat L Muntaha – mti unaomaliza mambo yote au mwisho wa mambo.
KWA NINI MAJINI NA WACHAWI HAWAPENDI MTI HUU?
Mti huu huwa unapendwa sana kukaliwa na malaika wakubwa kama RAUQAYAAIL, SAMSAMAAIL, GHANAAIL, ISRAHAMAAH, DARDAAIL.
Majini wote waasi na wachawi huwa wanapofika mahali penye mti wa mkunazi hawawezi kukaa wala kusimama mahala hapo na ndiyo maana Mkunazi unapo kuwepo basi katika nyumba hiyo huwa hafiki mchawi wala shetani.
FAIDA YA MKUNAZI
Majani yake ukiloweka na kuogea iwapo utasomea aya za qur aan basi utaepukwa na kukaliwa mbali majini aina 10 wakorofi ambao ni
Jalwush
Ummu muldami
Ankis
Ghaughaan
Bedui bidwaan
Makata wa makatani
Maymuna l hind’
Zawaabil
Atruush
Subyaan
Majini hao kamwe hawata mdhuru tena mtu iwapo atafanyia kisomo maalum cha KHAWAATIMU katika maji yaliyo lowekwa majani ya mkunazi.
2.Pia majani ya mkunazi iwapi unaumwa KIFUA SUGU lakini si pumu, chemsha pamoja na ndimu kisha unywe kwa siku 14 utapona.
3.Kama unawangiwa au kutembelewa na wachawi mara kwa mara basi chukua majani ya Mkunazi.
Weka HAIJALI na FAYJALI loweka pamoja na usomee kisomo cha KHAWAATIMU, kisha umwage ndani ya nyumba au shamba na wachawi hawatokujia tena kukudhuru.
4.Tabia ya mti huu ni ajabu sana kama ulivyo mti wa MZAYTUNI, mtu mwenye roho mbaya akipanda basi mti huu hauoti na mchawi akipita katika eneo lenye mti huo, basi ajue mtukuta asubuhi, na hatoondoka mpaka wachawi wenzake waje wamlipishe faini.
EmoticonEmoticon